HomeResourcesSabbath School quarterly
Hali Yetu
29/03/2026
Je, umewahi kujiuliza Yesu angesema nini kama angeelezea uhusiano wako Naye sasa hivi? Pengine angesema ni imara, au kwamba umekuwa imara zaidi huko nyuma. Je umewahi kujiuliza Yesu angesema nini akielezea juu ya watu Wake katika siku hii za mwisho? Katika Ufunuo 3: 14-22, Yesu kwa hakika anaielezea.
Anaanza kwa kusema kwamba Yeye ni “ ‘ “Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu” ’ ” (Ufu. 3:14). Shahidi mwaminifu na wa kweli hasemi uongo bali husema wazi na kwa uaminifu.
Bwana Yesu anatuambia, Wakristo katika siku za mwisho, kwamba anatujua. Sisi si moto au baridi, kwa sababu, kutokana na mtazamo wetu, hatuhitaji chochote. Siku na majuma hupita, na tunatumia muda kidogo na Mungu hapa na pale, na tunafikiri hiyo inatosha. Lakini sivyo. Badala yake, kwa kweli tunamhitaji sana kuliko tunavyotambua. Laiti tungeweza kumpenda na kuishi kwa ajili ya Yesu kwa moyo wote au la kabisa. Hiyo ingekuwa bora kutokana na mtazamo wa Mungu kuliko kuwa vuguvugu. Yesu anasema kwamba atatutapika kutoka kinywani Mwake kwa sababu tuna ladha mbaya kama tulivyo. Lakini bado hajafanya hivi, na anatuomba tufanye maamuzi ya ujasiri sasa hivi.
Katika nyakati za kale, “kununua” kitu kulimaanisha kubadilishana au kubadilishana bidhaa. Hapa, Yesu anakaribisha zoezi la kubadilishana: hali yetu ya kutojali kubadilishana na dhahabu Yake, na mavazi Yake meupe, na dawa Yake ya macho. Anataka kutufanya matajiri machoni Pake; Anataka kutufunika vazi Lake kamilifu la haki; na anataka kufungua macho yetu kuona ukweli wa jinsi uhusiano wa kudumu pamoja Naye utakavyobadilisha kila kitu kabisa. Anatupatia yote tunayohitaji, hasa kwa sababu kile tunachohitaji, hatuwezi kujipatia wenyewe. Yeye peke Yake anaweza na atafanya, lakini ikiwa tu tuna nia.