HomeResourcesSabbath School quarterly
Jifunze zaidi
01/05/2026
Kusudio la kujifunza Biblia ni kumjua Mungu na kukua katika uhusiano wako na Yeye, kwani huu ndio uzima wa milele — kuwa milele pamoja na Mungu tunayempenda (Yohana 5:39; Yohana 17:3).
Sehemu ya uhusiano wowote ni ushiriki wa pande zote husika. Tunasoma katika Ufunuo 3:20 kwamba Yesu anataka hili liwe kati Yake nasi, hata hivyo ni lazima tutambue kwamba, kama viumbe vilivyoumbwa, daima tunaweza kujifunza zaidi kuhusu Muumba wetu. Kama mchimba migodi anayechimbua vito vya thamani, tunapaswa kutafuta daima katika Biblia. Daima kuna mengi ya kukusanya, haijalishi ni mara ngapi tumesoma visa fulani au aya za Biblia. “Hata mtu awe ameendelea kiasi gani, asifikirie hata kidogo kwamba hakuna haja ya kuchunguza Maandiko kwa kina na kuendelea kupata nuru kubwa zaidi. Kama watu, tunaitwa mmoja mmoja kuwa wanafunzi wa unabii.” —Ellen G. White, Counsels to Writers and Editors, uk. 41.
Hatupaswi pia kujaribu kuifanya Biblia ilingane na maoni au mawazo yetu ya kibinadamu. “Tutachunguzaje Maandiko?” Je, tunawezaje kuweka viwango vyetu vya mafundisho kimoja baada ya kingine, na kisha tujaribu kufanya Maandiko yote kukidhi maoni yetu? Au tuchukue mawazo na maoni yetu kwa Maandiko, na kupima nadharia zetu kwa kila upande kulingana na Maandiko ya kweli? Wengi wanaosoma na hata kufundisha Biblia, hawaielewi kweli yenye thamani wanayoifundisha au kujifunza.... Wengi huyapa maneno Maandiko maana inayolingana na maoni yao wenyewe.” —Ellen G. White, Counsels to Writers and Editors, uk. 36.
Masawali ya Kujadili
Muhtasari: Kujifunza Biblia kwa mtu binafsi ni kiini cha kuwa na uhusiano ulio hai na unaodumu pamoja na Mungu. Neno la Mungu liko hai kwa namna yenye manufaa katika karne ya ishirini na moja, kama ambavyo limekuwa katika karne zilizopita. Kwa namna hiyo hiyo ya kudumisha uhai wa urafiki, yatupasa tutafute njia za kudumisha maisha yetu ya ibada yakiwa wazi tunapodumu katika Yesu, tukiamini ahadi Yake aliyosema kwamba, “Neno langu,...litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” (Isa. 55:11).