HomeResourcesSabbath School quarterly
Jifunze zaidi
19/06/2026
“Haidhuru uwe na taaluma gani, hakuna mtu mwenye upendo safi kwa Mungu isipokuwa ana upendo usio na ubinafsi kwa ndugu yake. Lakini hatuwezi kuipata roho hii kwa kujaribu kuwapenda wengine. Kinachohitajika ni upendo wa Kristo moyoni. Wakati nafsi inapounganishwa ndani ya Kristo, upendo hujitokeza wenyewe.”—Ellen G. White, Christs Object uk 384
“Wale wanaojishughulisha kwa bidii na kwa uaminifu wa moyo wote katika kazi ya kuwaleta watu kwa Yesu Kristo, ndio waliokomaa zaidi katika maisha ya kiroho na ibada.”—Ellen G. White, Evangelism, uk. 356.
“Nguvu ya kupinga uovu hupatikana kwa kujitoa kwa bidii kumtumikia Mungu.”—Ellen G. White, The Acts of the Apostles, uk. 105.
“Ili kuingia katika furaha Yake—furaha ya kuona roho zikikombolewa kwa dhabihu Yake—tunapaswa tushiriki katika Kazi yake ya kuwakomboa.”—Ellen G. White, The Desire of Ages, uk 142
“Wale wanaokataa fursa ya kushirikiana na Kristo katika huduma, wanakataa mafunzo pekee yanayowafanya kustahili kushiriki pamoja Naye katika utukufu Wake.”—Ellen G. White, Education, uk. 264.
Masawali ya Kujadili
Muhtasari: Upendo wa Mungu na Neno Lake lililo hai na lenye nguvu vinapojaza maisha yetu ya kila siku, tutasukumwa kumpenda na kumshuhudia kwa wale wanaotuzunguka. unapaswa kuwa watu wa maombi, wenye kutafakari, na wenye kusudi katika kushuhudia, tukiamini kwamba Neno Lake, litokalo katika kinywa Chake, halitarudi Kwake bure, bali litatimiza mapenzi Yake, na litafanikiwa katika jambo ambalo amelituma (tazama Isaya 55:11).